Desemba tarehe nne ndio miungano kamili itakuwa imekamilika, tayari kwa uchaguzi mkuu ujao. Na huku vigogo wa siasa wakipanga na kupangua, mbinu zinazoshika kasi sasa ni zile za tenga utawale. Msimamo huu ulipata utetezi kufuatia mabadiliko katika baraza la mawaziri. Bendera zilizawadiwa wale walioonekana ni waaminifu, lakini wachambuzi wa siasa wanasema kuna kubwa zaidi. Waziri mkuu akionekana amechacha na mkakati wa kulidhibiti eneo la magharibi, na rais kibaki pengine akituma ujumbe ule mradi wake wa chaguo lake bado upo jikoni. Kufaulu kwa mikakati hii