Katika siku za hivi karibuni,mandhari ya barabara zilinyooka bila viraka vya lami imekuwa ya kutizamwa katika pembe nyingi za nchi. Na leo,uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara wa shilingi bilioni nne ulizinduliwa eneo la Nanyuki kaunti ya Laikipia .waziri wa barabara Franklyn Bett alipongeza raia kwa kuhusika kwenye ujenzi wa aina hiyo kwani ni mara ya kwanza kwa wenyeji wa eneo fulani kuhusishwa kwenye ujenzi wa barabara yoyote. Ni mradi ambao umehusisha serikali ya kenya na ile ya ufaransa na tayari kilomita zaidi ya elfu moja zimejengwa chini ya mradi huu awamu ya kwanza. Kaunti sita na maeneo bunge 31 eneo la kati na Rift Valley yatafaidika kutokana na