Mbunge wa kajiado kusini katoo ole metito ndio sasa waziri mpya wa usalama wa ndani. Katika mabadiliko ya baraza la mawaziri rais mwai kibaki na waziri mkuu raila odinga pia walimteua mbunge wa budalangi ababu namwamba kama waziri mpya wa michezo. Namwamba anachukua mahali pa paul otuoma ambaye amehamishiwa wizara ya serikali za wilaya. Mbunge wa mugirango magharibi john gesami amerejea kama naibu waziri wa matibabu baada ya kuondolewa mashtaka ya ufisadi.