Waziri wa mazingira Chirau Ali Mwakwere anayekabiliwa na kesi ya uchochezi, leo amejirudi na kuomba msamaha. Akionekana kukiri matamshi hayo ya uchochezi, mwakwere aliomba msamaha wake mbele ya wanaharakati wa shirika la muhuri, ambalo ndilo lililowasilisha malalamishi mbele ya tume ya utangamano ncic. Mwenyekiti anayeondoka wa NCIC mzalendo kibunjia alikataa kuzungumzia ombi hili la msamaha la mwakwere akisema muda wake wa kuhudumu ulimalizika jana. Mbunge huyo wa matuga anakabiliwa na kesi mahakamani, na akipatikana na hatia huenda akapoteza bendera yake ya mazingira