Chimbuko la asili ya jamii humu nchini, huchangia pakubwa katika miegemeo ya kisiasa na vile vile namna jamii zinavyopiga kura humu nchini. Wasomi wa kihistoria wanasema usishangae kuwaona wabantu wakihangaishwa na kuwa na kigogo mmoja, kwani asili yao si watu mbali hujitokeza kuwa wababe wa jamii hizo. Ukiziangalia jamii za maeneo ya ziwa au mito , ama zile za wafugaji hufuata nyayo za kigogo mmoja, bila tatizo. Wachambuzi wa kisiasa lakini wanakosoa mtazamo huu, wakishikilia kuna vivutio vingine ambavyo huwa ndio muamuzi wa namna maeneo mbali mbali hujigamba kisiasa. Mzizi wa siasa za humu nchini ndio makala ya leo ya kingang’anyiro