Wenyeji wa Maralal mwaka huu watakuwa wakiadhimisha miaka ishirini na mitatu tokea kuanzishwa kwa mashindano ya ngamia almaarufu camel derby. Mashindano hayo yamefika tena eneo hilo lengo kuu likiwa ni kuhubiri amani. Kila wakati kumekuwa kukiripotiwa mzozo baina ya jamii tofauti tofauti, swali ibuka sasa ni je, mashindano hayo yatafanikiwa kusitisha ule wizi wa mifugo unaowakabili wenyeji kila wakati?