Wanamgambo sabini na watatu wa kundi la kigaidi la Alshabab wameripotiwa kuuawa katika eneo la fafahdun katika nchi jirani ya Somalia. Mashambulizi hayo yanajiri siku chache tu baada ya helikopta tatu za wanajeshi wa Uganda kuhusika katika ajali katika msitu wa mlima Kenya. Miili mingine mitano imepatikana katika eneo la ajali asubuhi ya leo. Na kama anavyotuarifu mwanahabari wetu Mohamed Mahmoud, ndege hizo tatu zilitarajiwa kusaidia pakubwa katika mashambulizi dhidi ya wanamgambo hao katika mji wa Kismayo, ambayo ndio ngome yao kuu.