Mtazamaji si siri kwamba safari ya wakenya ya kusaka tume itakayohakikishia taifa uchaguzi wa huru na haki imekuwa na yenye pandashuka nyingi.katiba ilipopitishwa wengi walijawa na matumaini kuwa hatimaye tume huru ya uchaguzi IEBC ingeleta mabadiliko makuu, lakini malumbano ambayo yamekuwepo baina ya makamishna ya tume hiyo kuambatana na zabuni ya sajili za elektroniki kufikia upeo wa kutwika serikali jukumuhilo imewatamausha wengi, suala likiwa je tume ya iebc imepoteza uhuru wake? Na je kuna haja ya wakenya kuendelea kuiamini tume hiyo?ndio hoja inayotupambia makala uyapendayo ya kila ijumaa ya kinyanganyiro.