Je ni nani anayewauwa madereva wa teksi na kisha kutupa maiti zao eneo la Nairobi West? Ni maafa ambayo maafisa wa polisi wa kituo cha polisi cha langata wameshindwa kukomesha au hata kuwatia washukiwa nguvuni .kwa muda miezi mitatu sasa madereva wa teksi tisa wamepatikana wameuwa na kutupwa karibu na shule ya msingi ya madaraka.wote wameuawa kwa kupigwa mawe kichwani na watu wasiojulikana . Muthiriwa wa hivi majuzi ni Vincent Mburu ambaye kifo chake kimewaacha madereva wa teksi na wasi wasi mwingi.