Hatimaye naibu jaji mkuu aliyesimamishwa kazi Nancy Baraza amekata rufaa dhidi ya uamuzi wa jopo kumtimua kutoka wadhifa wake huo. Kupitia wakili wake Kioko Kilokumi, Baraza alisema hajatosheka na uamuzi huo. Jopo hilo lililoongozwa na jaji mstaafu augustino ramadhan lilitoa mapendekezo kwa rais kwamba baraza apigwe kalamu kwa kukiuka maadili ya afisa mkuu serikalini. Hii ni baada ya kudaiwa kumtishia maisha mlinda lango Rebeca Kerubo huko village market mwezi Desemba mwaka jana.