Leo ni Agosti tarehe saba, ikiwa ni siku ya maadhimisho ya waathiriwa wa mkasa wa mlipuko wa bomu, uliotokea hapa Nairobi mnamo mwaka wa 1998. Lakini anavyoripoti Frank Otieno, familia hizo zinahisi upweke kutokana na jinsi serikali inaonekana kunyamaza kuhusu maadhimisho hayo; kwani hii leo walijikusanya kimyakimya wakiwa hapa jijini Nairobi na kuwakumbuka wapendwa wao.