Ndege moja aina ya helikopta ilianguka ghafla baada ya kusemekana kupata matatizo ya kimitambo na kusababisha kujeruhiwa kwa rubani wawili waliokuwemo ndani ya ndege hiyo. Marubani hao waliokuwa wakitoka kusini mwa Sudan katika eneo la Juba walinusurika vifo na badala yake kupata majeraha madogo madogo.