Waziri mkuu raila odinga amesema hana haja ya kujibizana na aliyekuwa mshauri wake wa zamani- Miguna Miguna. Raila ameyasema hayo hivi leo katika eneo bunge lake la Langata, alipowahutubia wafuasi wake katika uwanja wa Kamukunji huko Kibera. Frank Otieno ametuandalia taarifa hiyo ya kampeini za kisiasa, ambapo hii leo Raila na Musalia Mudavadi wamefanya kampeini tofauti hapa nairobi.