Tume ya IEBC imeshauriwa na baraza la mawaziri kurejelea mfumo wa kupiga kura wa elektrokini ambao ulitupiliwa mbali siku ya jumatano na tume hiyo. Mzozo unaohusu zabuni uliipelekea tume hiyo kurejelea mfumo wa awali wa kupiga kura. Baraza hilo linadai kuwa mfumo wa elektroniki utahakikisha uwepo wa uchaguzi huru na wa haki katika uchaguzi mkuu ujao.