Watumishi wa umma wenye nia ya kugombea nyadhifa mbalimbali za siasa kwenye uchaguzi mkuu ujao wanafaa wang'atuke afisini ifikapo mwezi septemba mwaka huu. Mahakama kuu imetupilia mbali kesi iliyowasilishwa mbele yake na mwanaharakati charles omanga kupinga makataa ya miezi sita iliyotolewa na katiba. Katika uamuzi wake jaji isaac lenaola amesema muda huo unatosha kwa afisa yeyote kwenye utumishi wa umma kujiondoa na kuanza kampeni zake.