Mgogoro umeibuka kati ya kampuni ya huduma za maji jijini mombasa na wauza maji wa mikokoteni mjini humo. Kampuni hiyo inataka baadhi ya vioski vya kuuza maji vifungwe. Lakini muungano wa wauza maji mombasa unadai, wao ndio tegemeo la wakazi wa mombasa, na hivyo onyo la kampuni ya huduma za maji mombasa kufunga vioski vyao litawaacha wakazi wengi bila maji. John juma na taarifa zaidi kuhusu kisiwa kinachozingirwa na bahari lakini hakiwezi kukidhi mahitaji ya maji kwa wakazi wake kikamilifu