Hakuna haja ya kukagua wasafiri katika mipaka ya kuingia Kenya kupitia Malaba na Busia. Ni kauli yake Mkurugenzi wa afya ya umma shahnaaz shariff akisema kuwa hakuna haja ya wanachi kuwa na hofu yoyote huku serikali ikiimarisha hali ya afya katika maeneo hayo. Hata hivyo vituo vya mabasi ya kueleka uganda vingali na wateja chungu nzima ila kuna upungufu wa wasafiri kutoka nchi ya Uganda wanaoingia Kenya. Mwanahabari Saida Swaleh na taarifa hiyo.