Watu kumi na wanne wamefariki magharibi mwa Uganda katika wilaya ya Kibaale iliopo kilomita 170 kutoka jiji la Kampala baada ya kuambukizwa maradhi ya ugonjwa wa Ebola. Mmoja kati ya waliofariki,aliaga dunia jijini Kampala huku Rais Yoweri Museveni akionya Mataifa jirani kujikinga dhidi ya maambukizi ya Ebola . Watu wengine wanaoshukiwa kuwa na virusi vyaEbola wametengwa kutoka hospitali kuu ya Mulago kwa hofu ya maambukizi zaidi. Mwahabari Saida Swaleh na taarifa hiyo.