Vinara wa tume ya kitaifa ya haki za binadamu pamoja na taasisi ya masuala ya elimu na demokrasia, I.E.D., wanamtaka waziri wa sheria Eugene Wamalwa kuharakisha utaratibu wa kumteua msajili wa vyama vya siasa haraka iwezekanavyo ili kuweka nidhamu katika ulingo wa siasa. Samuel Tororei na Peter Aling’o wanasema hatua ya serikali kuchelewesha mipango ya kuteua rasmi msajili wa vyama imepelekea baadhi ya wanasiasa kuvunja sheria ya vyama kiholela, huku vyama vingine vikipokea vyeti vya usajili kwa kutumia mbinu za ujanja.