Watu wanne wamefariki Jumamosi huko Mombasa katika ajali mbili tofauti tofauti. Maafa hayo yameweka idadi ya wale waliokufa Mombasa mwezi huu pekee kuwa zaidi ya ishirini. Ajabu ni kuwa ajali zimetokea katika maeneo ambayo yameorodheshwa kuwa hatari. Ndiposa tunauliza swali je watumizi wote wa barabara wanatilia maanani maeneo hatari. John Juma anaangazia baadhi ya maeneo hayo hatari barabarani Mombasa kutahadharisha dhidi ya maafa zaidi.