Baada ya watu watano kufariki ndani ya bohari mjini mombasa mapema wiki hii walipoporomokewa na magunia ya mchele, sasa inabainika kuwa bohari nyingi nchini hasa mombasa hazikaguliwi kamwe na serikali. Hali hiyo imeacha maisha ya wafanyikazi wengi kuwa katika hatari kubwa. Kadhalika hali hiyo imeruhusu biashara nyingi haramu mfano ulanguzi wa mihadarati kuendeshwa kisiri. Maafisa wa polisi nao wanalaumiwa kupokea hongo kutoka kwa wamiliki wa bohari hizo ili kuficha ukweli kila wafanyikazi wanapotaka kufichua. John juma anapigia darubini masaibu ya wafanyikazi na uvundo uliofichika katika bohari za mombasa