Triza Wanjiru mkewe bingwa wa mbio za nyika marehemu Samuel Wanjiriu amejitokeza wazi kukana uhusiano wa kimapenzi na aliyekuwa kiongozi wa kundi haramu la mungiki Maina Njenga wala hajawahi kuolewa naye. Kulingana na Triza maisha yake yamo hatarini kwani kuna watu wanaomuandama na kutaka kumchafulia jina ili itumiwe kama ushahidi wa kesi dhidi yake Mahakamani. Wakili wake atawasilisha barua ya kutaka wale waliochapisha habari hio kupitia ripoti iliyoandikwa na kutolewa na kampuni moja ya mtandao inayofahamika kama Daily Post nchini Kenya kwenye tarakilishi kutoa ushahidi wa ndoa baina yake na Maina Njenga.