Hayuko nchini na makaazi yake mapya ni kitendawili, lakini Miguna Miguna ndio alikuwa gumzo la Nyando, eneo, alikozaliwa. Wenyeji wakiongozwa na mbunge wao, Fred Outa waliingia mjini kudhihrisha ghadhabu zao dhidi ya Miguna Miguna na kitabu chake cha Peeling Back the Mask, kinachomlimbikizia kila aina ya sifa mbaya kinara wa ODM Raila Odinga. Hawakusaza machungu yao, walibeba sanamu ya Miguna na kuiteketeza moto, lakini ari yao ya kuizika sanamu hiyo nyumbani kwa kakake miguna, ilikatizwa na maafisa wa polisi. Na sasa kakaake eric miguna anaitaka serikali kuwapa usalama kutokana na vitisho wanavyovipokea.