Huku benki kuu ya Kenya ikitoa maeelekezo ya wazi kuhusu riba tunayopaswa kuchukua katika soko humu nchini , benki za biashara zimechelea kujibu wiki mbili baada ya kamati ya fedha kupunguza misingi ya mikopo kutoka asilimia 18 hadi asilimia 16.5. Kwa sasa ni benki kumi tu ndizo zimepunguza viwango vya riba.Hii sasa imezua wasiwasi kwa wakopaji wengi ambao wamekuwa wakipambana na bei ya juu ya riba. Hivi sasa kenya ina zaidi ya benki 45 ziliyo na leseni ,huku sita kati yao wakiwa na sehemu kubwa ya soko humu nchini, benki za kutajwa kama vile equity, benki ya KCB,benki ya national na ile ya cooperative hazijatoa dalili zozote za kupungua kwa viwango vya riba