Kampuni ya Coca Cola mapema hii leo imetangaza ufadhili wa shilingi milioni tano kwa timu ya olimpiki.Timu hiyo ambayo iko kambini katika uwanja wa kasarani ilikuwa na bajeti ya nusu bilioni na kujitokeza kwa Coca Cola kutasaidia pakubwa timu hiyo. Aidha kampuni hiyo imetangaza kuandalia timu hiyo karamu pindi tu watakapowasili nchini uingereza. Hafla hiyo ilihudhuriwa na maafisa wa shirikisho la olimpiki nchini Nock wenzao wa Athletics Kenya na wanariadha wa timu hiyo.timu hiyo ilikabihidwa cheki hiyo na meneja wa kampuni ya Coca Cola Rocky Findley.