Halmashauri ya KRA imetibua njama ya kuingiza humu nchini mbolea inayotumika kutengenezea vilipuzi. Maafisa wa kra walinasa kilo 20 za potassium nitrate na kilo 20 za sodium baada ya kufanya msako katika bohari moja katika eneo la mpakani huko namanga. Kulingana na afisa wa mauzo wa kra, watu wawili walijaribu kuwahonga maafisa wake, wasikague mzigo wao, waliokuwa wausafirishe katika basi la abiria. Mara ya kwanza kwa bomu kutengenezwa kwa mbolea ilijitokeza baada ya ule mlipuko wa jengo moja katikati mwa jiji la nairobi.