Mtangazaji mpekuzi wa makala yaliosifika kotekote nchini Jicho Pevu anatarajiwa kuondoka KTN ifikapo mwezi Agosti .Mohammed Ali anaondoka baada ya kuhudumia Shirika hili kwa muda wa miaka sita , wasifu wa Mohammed Ali unatokana na ujasiri wake wa kudhihirisha maovu yaliokomaa katika jamii kuanzia ufisadi , utapeli , wizi na hivi maajuzi makala yaliozuzua nchi ,yale ya Parwanja La Mihadarati , taarifa kutoka kwa shirika la Standard Group zadokeza kuwa Mohammed Ali alikuwa chombo muhimu kwa shirika hili lakini baada ya mazungumzo ya hawakuwa na budi ila kumruhusu kuendeleza taaluma yake kwengineko.