Je, mswada dhidi ya ugaidi utatoa suluhu kwa Taifa la Kenya? Ni suala linaloninginia kwenye fikra za wengi, huku baadhi wakitumai kuwa kupitia sheria hiyo mashambulizi ya kigaidi ambayo yamekuwa yakishuhudiwa Nchini yatatiliwa kikomo. Lakini viongozi wa dini ya kiIslamu na Mashirika ya Umma wanahisi kuwa kwa suluhu kupatikana sheria hiyo inahitaji kufanyiwa marekebisho kabla ya kufikishwa Bungeni. Kwa mujibu wao ni kuwa kielelezo cha Sheria hiyo kinakiuka haki za kimsingi zilizonakiliwa chini ya Katiba mpya.