Makamu wa Rais Kalonzo Musyoka amesema waKenya wanastahili kupiga msasa viongozi wanaowania nyadhifa tofauti ili kuwachagua viongozi waaminifu na wenye maadili mema. Kalonzo amesema kuwa baadhi ya wanasiasa wanaowania Urais, ambao hakuwataja kwa majina, wanajihusisha na siasa za uhuni kwa kujipigia debe kama wana mageuzi ilhali si watu wa kuaminika. Kwa upande wake mwenyekiti wa tume ya uwiano Mzalendo Kibunjia amewataka wapiga kura kupiga kalamu viongozi wanaoeneza chuki na uhasama miongoni mwa jamii.