Mbabe wa kivita kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo Thomas Lubanga ndiye amekuwa mtuhumiwa wa kwanza kuhukumiwa na mahakama ya kimataifa ya jinai ya ICC.Mahakama hio imemfunga Lubanga kifungo cha miaka 14 ,Hukumu hiyo ilitolewa asubuhi ya leo baada ya Lubanga kupatikana na hatia ya kuwatumia vijana wadogo kama wanajeshi kati ya mwaka 2002 na 2003 Kaskazini mwa Nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo.