Kufuatia ongezeko la visa vya mashambulizi katika makanisa kisa cha hivi maajuzi kikiwa cha shambulizi kwenye makanisa mawili mjini Garissa ambapo watu 17 waliaga dunia na wengine takribani 60 kujeruhiwa vibaya, makanisa mbali mbali nchini yameimarisha usalama kwa kuhakikisha kuwa waumini wanakaguliwa na hata wengine kulazimishwa kutoingia kanisani na mikoba yao .