Wakongwe walioshiriki vita vya maumau nchini wameitaka serikali ya Kenya kuwapa msaada wa kifedha kusaidia katika kesi wanayowasilisha dhidi ya serikali ya uingereza kuhusu mateso waliyopitia chini ya uongozi wa mkoloni kabla ya kenya kupata uhuru.wakongwe hao wakiongozwa na tume ya kutetea haki za kibinadam nchini wametangaza safari ya kusikizwa kwa awamu ya pili ya kesi yao baada ya mahakama kuu ya uingereza kuwapa ruhusa ya kuishtaki Uingereza.