Nchi ya Saudi Arabia inapotajwa nchini Kenya huleta taswira mbili kwanza ya tabasamu kwani ndio kitega uchumi kwa wengi na huzuni kwani imeacha makovu katika nyoyo za wakenya wengi waliosafiri huko. Lakini hivi karibuni serikali ilipiga marufuku usafiri wa nchi za Uarabuni hadi pale itakaposuluhisha swala la dhuluma miongoni mwa wakenya wanaofanya kazi huko. Lakini swala la serikali kutoa mikakati ya kuwahamisha wale waliosalia huko na kupitia mateso limesalia kuwa kitendawili na hii leo KTN imelivalia njuga swala hili na kupata picha za kipekee ambazo ziliweza kutumwa na wakenya waliozuiliwa katika vituo kadhaa, Saudi Arabia. Je nani atakuwa mkomboziwao? Huku kilio chao kikiwa ni serikali kuwarudisha humu nyumbani.