Afisi ya kiongozi wa mashtaka wa mahakama ya ICC na naibu waziri mkuu Uhuru Kenyatta wameafikiana kuhusu mfumo utakaotumiwa kutoa ushahidi ulio mikononi mwao kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi yake. Hata hivyo aliyekuwa mkuu wa utumishi kwa umma Francis Muthaura amepinga mapendekezo yaliyotolewa na kutaka arafa zote katika stakabadhi za ushahidi kujumuishwa. Nao upande wa mashtaka umepinga wito huo kwa kusema kuwa hilo haliwezekani hadi pale kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.