Kamishna wa Polisi Mathew Iteere amepinga madai kuwa Idara ya Usalama ilifahamu kuhusiana na shambulizi la jana na ikakosa kuchukua hatua mwafaka. Iteere amesema kuwa maafisa wa polisi walikuwa tayari wameshika doria katika maeneeo yaliyolengwa ili kuimarisha usalama. Idara hiyo imepata utetezi kutoka kwa Waziri Mkuu Raila Odinga ambaye amesema kuwa iwapo mauaji ya maafisa wawili wa polisi katika shambulizi hilo ni ishara kwamba hatua zilikuwa zimechukuliwa.Waziri Mkuu pia ametangaza kuwa mashambulizi yanayoendelea hayatofanya serikali kuoondoa majeshi yake kutoka nchini Somali wala kuingia hofu.