Kongamano la siku tatu la vijana wa Bara La Afrika limefunguliwa leo Gigiri, katika makao makuu ya umoja wa mataifa hapa jijini Nairobi. Maudhui makuu ya kongamano hilo ni mbinu za vijana kujitolea kudumisha amani na kuimarisha maendeleo barani Afrika. Shirika la Standard Group limeshirikiana na Wadau wengine kufanikisha Kongamano hilo linalohudhuriwa na washiriki kutoka Kaunti zote arobaini na saba nchini, pamoja na wageni kutoka nchi za Bara la Afrika, vijana humu nchini wakitakiwa kudumisha amani wakati huu Kenya inapokaribia Uchaguzi mkuu.