Wanariadha wote wa Kenya ambao wanajiandaa kwa mashindano ya olimpiki wamefika kwenye kambi ya mazoezi kasarani. Na kujiunga na kocha mkuu Julius Kirwa, mazoezi rasmi yataanza jumatatu katika uwanja wa kasarani. Lakini huku timu ya Kenya ikijiandaa, swala tata la baadhi ya wanariadha kutakikana kusafiri siku ya jumanne hadi Bristol, Uingereza bado halijatatuliwa.