Baada ya uamuzi wa mahakama kuhusiana na uteuzi wa wakuu au makamishna wa maeneo 47 ya kaunty , hii leo hisia tofauti zimeibuka kuhusiana na iwapo wanafaa waendelee kuweko au la, licha ya uamuzi wa mahakama hii leo makamishna hao walikuwa kweney mkutano spesheli ili kufunzwa zaidi kuhusiana na usimamizi wa kaunty ambapo kaimu mkuu wa utumishi nchini francis kimemia amedokeza kuwa hakutakuwa na migongano kati ya ofisi ya magavana na ile ya makamishna wa serikali , huku hayo yakijiri ni wazi kuwa swala hili la uteuzi wa makamishna limezungukwa na utata kwani huku waziri wa sheria za katiba eugene wamalwa akidokeza kuwa haungi mkono uwepo wao , katibu wa idara ya usalama naye amedokeza kuwa makamishna hao wataendelea kusimamia nydhifa zao , makamishna hao walikuwa katika chuo cha mafunzo ya uongozi kma mchana kutwa