Waziri wa huduma za afya Proffessa Anyang’ Nyongo amepuuzilia mbali sakata inayohusishwa na ufujaji wa fedha katika bima ya afya ya kitaifa NHIF . Nyongo anasema kuwa sakata hiyo imebuniwa na watu wanaotaka kuvuruga utenda kazi katiika bima hiyo . Akizungumza katika hospitali kuu ya kenyatta katika hafla ya k upewa kwa hospitali hiyo hati ya iso Nyong’o amedai kuwa hakuna mfanyikazi wa umma hata mmoja aliyejitokeza kulalamika kuhusu utendakazi wa nhif .