Kaimu waziri wa usalama wa ndani mohamed Yusuf Haji amewataka wanasiasa kukoma kueneza uvumi kuhusu kilichosababisha ajali ya ndege iliyowaua mawaziri George Saitoiti, Orwa Ojode pamoja na maafisa wanne wa polisi. Haji ametoa mwito kwa yeyote mwenye habari kuhusu ajali hiyo kuiwasilisha kwa tume iliyobuniwa kuchunguza ajali hiyo. Aidha, Haji amepinga madai eti uchunguzi wa ajali hiyo umecheleweshwa huku akisema mabaki ya ndege hiyo aina ya helikopta yataondolewa eneo la ajali wiki ijayo.