Henry Kosgey sasa ameondolewa mashtaka yaliyohusiana na madai ya kuingizwa kwa magari makuukuu humu nchini ,Mahakama imesema kwamba wakati alipoidhinisha kuagizwa kwa magari hayo sheria kuhusiana na uzee wa magari haikuwa imeanza kutumiwa.hatua hii sasa inamfufua kisiasa na inawadia wakati ambapo amekuwa akimshinikiza Raila Odinga kumteua kama mgombeaji mwenza.swali tunaloliuliza ni iwapo chama cha ODM sasa kitampa wadhifa huo?