Huku Kenya ikikaribia uchaguzi mkuu ujao, tetesi zimechipuka kwamba wapo baadhi ya wasanii wanaotunga nyimbo zinazohatarisha kuwagawanya Wakenya kwa misingi ya kupalilia kwekwe za uhasama. Kutokana na hilo Tume ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa( NCIC) inayoongozwa na Mzalendo Kibunjia imetoa onyo kali kwamba itawachukulia hatua kali wanamuziki wa aina hiyo pamoja na vyombo vya habari vitakavyoshiriki katika kuzipeperusha nyimbo hizo.