Familia ya marehemu Prof. GeorgeSaitoti kupitia wakili wao Fred Ngatia imelalamikia vikali kucheleweshwa kwa uchunguzi wa ajali ya helikopta iliyomuua Saitoti pamoja na naibu wake Orwa Ojode mnamo Juni tarehe kumi mwaka huu wa 2012. Lalama hizo zimejitokeza pale wakili huyo pamoja na nduguze marehemu Saitoti walipotembelea eneo la mkasa huo katika Kibiku katika msitu wa Ngong.