Zaidi ya nyumba kumi na tano zimefunikwa kutokana na kuporomoka kwa ardhi katika sehemu ya Bugisu karibu na mpaka wa Kenya na Uganda. Idadi ya watu waliofariki kutokana na maporomoko hayo bado haijadhibitishwa. Hata hivyo inahofiwa kuwa idadi kubwa ya wakaazi wa sehemu hizo imeangamia kwenye mkasa huo.