chama cha URP kimewashambulia wanasiasa wanaoshinikiza maswala ya ICC wakidai ni njama ya kuwafungia nje ya uchaguzi mkuu ujao. Haya yalisemwa huku naibu waziri mkuu Musalia Mudavadi alipofanya kampeini yake katika eneo la Teso na kupuuzilia mbali semi hizo na kuwataka wakenya kujiepusha na viongozi wanaoeneza kampeini hizo.