Mlipuko wa grunedi uliofanyika huko Mshomoroni- Mombasa, umeiweka serikali katika hali ngumu ya kujaribu kuwashawishi wananchi na wageni kuhusu usalama wao. Waziri Mkuu Raila Odinga amesema kuwa tahadhari iliyotolewa na serikali ya Marekani kuhusu shambulizi hilo ishara kuwa idara ya ujasusi nchini Marekani ni ya kiwango cha juu. Frank Otieno anadadisi hali hiyo inayozua swali la je, serikali ilipopuuza onyo la Marekani na kisha grunedi likalipuka na kuwaua watu watatua,Wakenya waeleweje kuhusu usalama wa nchi yao?