Vikundi vinne vya kikosi cha Kenya cha olimpiki vitaondoka nchini julai 3 kuelekea jiji la Bristol nchini London kwa mazoezi maalumu mbele ya kuanza kwa mashindnao ya olimpiki julai 27. Timu ya mita 800, mita 1500, wana ndondi na wanariadha wa mbio za 4x400 relay zitaondoka julai tarehe tatu. Kikosi cha marathon ya wanaume kitakuwa wa mwisho kuondoka agosti 7. Hayo yalitangazwa wakati kambi ya mazoezi ilipofunguliwa rasmi na waziri wa michezo, Paul Otuoma.