Viongozi wakuu mbalimbali humu nchini wameshutumu vikali marekani kwa kutoa tahadhari kuwa mji wa Mombasa unatishiwa kushambuliwa kigaidi wakati wowote. Viongozi wa Kenya miongoni mwao makamu wa rais Kalonzo Musyoka, waziri wa utalii Dan Mwadzo na kaimu mkuu wa utumishi wa umma Francis Kimemia sasa wanataka marekani kufutilia mbali tahadhari hiyo na watangaze kuwa Mombasa na Kenya kwa jumla i salama.