Eneo bunge la Ugenya leo ndilo lilikuwa mwenyeji wa kumpa mkono wa buriani mmoja wa waathiriwa wa ule mkasa wa ajali ya ndege wa wiki iliopita. Kapteni Luke Oyugi alipewa heshima za mwisho zinazopewa maafisa wa polisi, katika mazishi hayo ambayo licha ya kutokuwa na wanasiasa, yalihudhuriwa na wakuu kadhaa wa polisi. Oyugi, alikuwa rubani msaidizi wa ile helikopta ya polisi ilioanguka na kuwaua Waziri wa Usalama Prof George Saitoti na Naibu wake Orwa Ojode. Mazishi ya oyugi yalifanyika huku chama cha marubani humu nchini leo kikitoa mwito wa kutaka kujumuishwa katika lile jopo la kuchunguza ajali hiyo. Jopo hilo lilikula kiapo hapo jana.