Unaweza kusamehewa unaposhuku ni ulipizaji kisasi. Simba wawili walikivamia kijiji kimoja, huko Kitengela, karibu na eneo ambalo jana simba sita waliowawa na vijana wa Kimoran. Kondoo wawili waliuawa katika uvamizi huo hii leo, huku wengine wanne wakiachwa na majeraha. Idara ya wanyama pori imepewa ilani ya kutatua uvamizi wa wanyama pori, la sivyo wenyeji wameamua watachukua sheria mikononi mwao.